• HABARI MPYA

    Friday, March 08, 2019

    AMUNIKE ANAMJUA ADI YUSUPH WA SOLIHUSS MOORS YA UINGEREZA

    Na Socrates W. Maganga, DAR ES SALAAM
    KOCHA wa Tanzania, Mnigeria Emmanuel Amunike ametaja kikosi cha Taifa Stars kitakachomenyana na Uganda katika mchezo wa mwisho wa Kundi L kufuzu Fainali za kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) Machi 24, mwaka huu Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.
    Amewaita wachezaji wote watatu wanaocheza Misri, viungo; Himid Mao wa Petrojet FC, Shiza Kichuya anayecheza kwa mkopo ENPPI kutoka Pharco FC ya huko pia na mshambuliaji Yahya Zayd wa Ismailia. 
    Taifa Stars itakuwa mwenyeji wa The Cranes Jumapili ya Machi 24 Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam katika mchezo wa mwisho wa Kundi L kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), siku ambayo Cape Verde watawakaribisha Lesotho Uwanja wa da Varzea mjini Praia katika mchezo mwingine wa kundi hilo. 

    Abdillah Yusuph kwa sasa anacheza Solihuss Moors ya Ligi Daraja la Nne Uingereza

    Tanzania inahitaji ushindi katika mchezo huo ili kujitengenezea mazingira ya kufuzu AFCON ya kwanza tangu mwaka 19980 nchini Nigeria.
    Lakini pia Watanzania watatakiwa kuiombea dua mbaya Lesotho isishinde mbele ya Cape Verde mjini Praia, kwani ikishinda itafuzu kutokana na wastani wake mzuri wa mabao na pia kubebwa kwa matokeo yake dhidi ya Taifa Stars.
    Kikosi kamili cha Taifa Stars; Makipa; Aishi Manula (Simba SC), Aaron Kalambo (Tanzania Prisons) na Metacha Mnata (Mbao FC).
    Mabeki; Suleiman Salula (Malindi SC), Hassan Kessy (Nkana FC - Zambia), Gardiel Michael (Yanga SC), Kelvin Yondan (Yanga SC), Vincent Philipo (Mbao FC), Ally Mtoni ‘Sonso’ (Lipuli FC), Andrew Vincent ‘Dante’ (Yanga SC), Kennedy Wilson (Singida United) na Aggrey Morris (Azam FC). 
    Viungo; Feisal Salum (Yanga SC), Jonas Mkude (Simba SC), Himid Mao (Petrojet FC - Misri), Mudathir Yahya (Azam FC), Shiza Kichuya (ENPPI - Misri), Simon Msuva (Difaa El Jadida – Morocco) na Farid Mussa (Tenerife B).
    Washambuliaji; Yahya Zayd (Ismailia - Misri), Shaaban Iddi Chilunda (CD Izara – Hispania), Rashid Mandawa (BDF XI - Botswana), Thomas Ulimwengu (JS Saoura - Algeria), John Bocco (Simba SC) na Mbwana Samatta (KRC Genk – Ubelgiji).  
    Naipenda Tanzania Napenda mpira na Naipenda stars kwa uelewa wa Kawaida tu Ni kwamba tunahitaji kupigana na Kufa kiume ili tuiue the cranes pale Kwa Mchina. Naunga mkono kwa maandalizi ya Tff na kamati shiriki zilizoandaliwa kwa ujumla na serikali pia.
    Lakini tunapaswa kujua ili tufanikiwe Ili tunahitaji Sana Kikosi kipana Ili timu iweze kufanya vizuri pia kuwepo na wachezaji professional kutoka katika ligi Bora za nje na ndani ya nchi huku tukiwekeza Vijana na ligi tukiwa serious kuliko Mapichapicha ya Sasa ilo halinihusu ngoja Nirudi kwenye hoja yangu ya msingi Super sub yangu ya Barcelona Fundi was mpira Emmanuel Amunike Unamjua Fundi Abdillah Yusuph..???
    Huyu jamaa anakipiga Solihuss Moors ya pale ligi daraja la nne Uingereza Ni Mbongo na Anajivunia Sana taifa lake. Amezaliwa 10 septemba 1992 akiwa na Umri wa Miaka 27 ana Urefu wa mita 181 na kilo 72 kg katika Msimu huu katupia goli 11 katika mechi 35 za mashindano Yote kwa ujumla Alianza soka lake katika academy ya Leicester city Mnamo Mwaka 2014.. Misimu wake wa Kwanza katika Maisha ya soka alisajiliwa na Oxford city Yaani 2014-2015 Huyu bwana Katika game 42 alizocheza alitupia Mabao 29 hivyo kufanya kudumu kwa Msimu Mmoja tu kabla ya kunyakuliwa kwa Ada ya usajili ya 2.1 million na Mansfield Town huku Alianza kucheza kwa mkopo na kufanya usajili wake kuwa wa jumla Maisha yalizidi kuenda Kasi na Umri ndio uliokuwa unahitaji mpira hivyo kila kitu kilikuwa kina kwenda kwa wakati Msimu huu alicheza game 30 tu na Kutokana na Majeraha aliyoyapa alitupia  Mabao 5 tu huku hatma Yake ikawa ngumu kutokana na ugumu wa  kugombea namba na Mastriker Waliokwenye peak Alietolewa kwa mkopo msimu wa 2016 kwenda Crewe Town ambapo alicheza game 23 akiwa ana maajabu Sana ya goli 5 Aliuzwa jumla na Mansfield kwenda Grimps Fity Fc ambapo alicheza Michezo 11 tu na kufunga goli 3 kawaida ya soka huwa linapanda na kushuka hivyo Basi Ni vigumu kuwa Bora kila wakati huku changamoto zikizidi kuandama kumuomba Mungu na kuongeza juhudi Ni chanzo Cha mafanikio Akukata tamaa na kuzaza huku akijua haina kufeli Alisajiliwa na barrow city 2017--2018 Ambapo alicheza game 25 nakufunga goli Kumi alicheza Nusu Msimu kabla ya kuendelea kuuwasha moto katika Msimu huu akionekana Kama Mshambuliaji hatari Sana katika league one Pale England Amekuwa akisifiwa na Makocha mbalimbali kutokana na uwezo wake wa kumiliki mipira na kufanya maamuzi hatari katika wakati sahiii huku akipenda miguu yake kuongea Sana kuliko Mdomo wake Ni mtu asiyependa Sana Makuu huku akiwa Ostadhi Balabala kutoka pale kidongo chekundu Zanzibar.Amunike ebu mtafute huyu mtu Nadhani kwa juhudi na experience alikuwa nayo Ni mtu sahihi wa kukaa na Fundi Mndengereko Mbwana samata.Kwa uelewa wangu mdogo tu Mwaka huu tusipo fanikiwa Tunabidi kwenda kwa Mzee Mwinyi kumuomba Msahamaha na kuuliza kwanii halituita Sisi kichwa Cha Mwendawazimu...? Siku zote Waswahili Usema kheri shati bovu kilo mgongo Wazi.Nasikia alishawahi kuitwa star ila hakucheza kutokana na Mechi ilifutwa kutokana na timu kuondolewa kwenye Mashindano.... Mwaka Wa mafanikio kwa sisi Wapenzi wa soka wa Tanzania Ni huu na Mda wetu ndo huu Tuisapoti taifa stars na Kujivunia Utanzania..
    (Socrates William Maganga anapatikana kwa namba 0655950100 au barua pepe williamssocrates@gmail.com)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AMUNIKE ANAMJUA ADI YUSUPH WA SOLIHUSS MOORS YA UINGEREZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top