• HABARI MPYA

    Saturday, February 09, 2019

    ARSENAL YAICHAPA HUDDERSFIELD 2-1, LAKINI YABAKI NAFASI YA SITA

    Kiungo Mnigeria, Alex Iwobi akishangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la kwanza dakika ya 16 katika ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, Huddersfield Town kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa John Smith mjini Huddersfield, West Yorkshire. Bao la pili limefungwa na Alexandre Lacazette dakika ya 44 kabla ya Sead Kolasinac kujifunga dakika ya 90 na ushei kuipa Huddersfield Town bao la kufutia machozi na kwa ushindi huo Arsenal inafikisha pointi 50, sawa na Chelsea baada ya kucheza mechi 26, ingawa inaendelea kushika nafasi ya sita 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL YAICHAPA HUDDERSFIELD 2-1, LAKINI YABAKI NAFASI YA SITA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top