• HABARI MPYA

    Thursday, December 06, 2018

    SUAREZ AFUNGA MAWILI BARCELONA YASHINDA 4-1 KOMBE LA MFALME

    Mshambuliaji Denis Suarez akipongezwa na wenzake baada ya kufunga mabao mawili dakika za 26 na 70 katika ushindi wa 4-1 dhidi ya Cultural Leonesa kwenye mchezo wa marudiano hatua ya 16 Bora Kombe la Mfalme Hispania usiku wa jana Uwanja wa Camp Nou. Mabao mengine ya Barca yalifungwa na Munir dakika ya18 na Malcom dakika ya 43, wakati la Cultural Leonesa lilifungwa na Josep Sene dakika ya 54. Barca inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 5-1 baada ya kushinda 1-0 ugenini kwenye mchezo wa kwanza 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUAREZ AFUNGA MAWILI BARCELONA YASHINDA 4-1 KOMBE LA MFALME Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top