• HABARI MPYA

    Wednesday, December 12, 2018

    SALAH AIPELEKA LIVERPOOL 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA

    Kocha Mjerumani wa Liverpool, Jurgen Klopp akimpongeza mshambuliaji wake Mmisri, Mohamed  Salah baada ya kuifungia bao pekee timu hiyo pekee dakika ya 34 ikiilaza 1-0 Napoli katika mchezo wa mwisho wa Kundi C Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa Anfield.
    Kwa ushindi huo, Liverpool inafikisha pointi tisa sawa na Napoli, ikimaliza nafasi ya pili kwa mabao mengi ya kufungam nyuma ya PSG iliyomaliza na pointi 11. Liverpool na PSG zinafuzu hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SALAH AIPELEKA LIVERPOOL 16 BORA LIGI YA MABINGWA ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top