• HABARI MPYA

    Wednesday, October 03, 2018

    JUMA ABDUL, AKILIMALI WAREJEA KUIONGEZEA NGUVU YANGA MECHI NA MBAO FC JUMAPILI TAIFA

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    BEKI wa kulia wa Yanga SC, Juma Abdul Jaffar Mnyamani aliyekuwa majeruhi tangu mwezi uliopita leo ameanza mazoezi kikamilifu na wenzake baada ya kupona.
    Abdul aliumia Agosti 23 katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu huu Yanga ikishinda 2-1 dhidi ya Mtibwa Sugar huku akitolewa dakika ya 89, nafasi yake ikichukuliwa na kiungo Said Juma ‘Makapu’.
    Mchezaji huyo Bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2015 – 2016, amekuwa akifanya mazoezi ya peke yake tangu wiki iliyopita na sasa yuko tayari kurejea uwanjani.
    Pamoja na Abdul, majeruhi mwingine, kiungo chipukizi Baruan Akilimali naye ameanza mazoezi leo baada ya kupona, hivyo kufanya Juma Mahadhi awe majeruhi pekee aliyebaki kwenye kikosi cha Yanga SC.

    Juma Abdul (kushoto) akitafuta maarifa ya kumpita mchezaji wa Mbeya City msimu uliopita

    Yanga SC inatarajiwa kuteremka uwanjani Jumapili Saa 1:00 usiku kumenyana na Mbao FC katika mfululizo wa Ligi Kuu Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam.
    Na leo Ofisa Habari wa klabu, Dissmas Ten ametangaza viingilio vya mchezo huo ambavyo vitakuwa Sh. 15, 000 kwa VIP A, 10,000 VIP B na C na Sh. 5,000 kwa majukwaa mengine yaliyobaki ya mzunguko.  
    Kwa ujumla Ligi Kuu inatarajiwa kuendelea Ijumaa kwa mchezo mmoja kati ya wenyeji, Lipuli ya Iringa dhidi ya Stand United Uwanja wa Samora.

    MECHI ZIJAZO LIGI KUU;
    Oktoba 5, 2018
    Lipuli v Stand United
    Oktoba 6, 2018
    Singida United v Ndanda FC
    Simba SC v African Lyon
    Kagera Sugar v Ruvu Shooting
    Tanzania Prisons v Mbeya City
    Mtibwa Sugar v KMC
    Oktoba 7, 2018
    Yanga SC v Mbao FC
    JKT Tanzania v Alliance FC
    Biashara v Nwadui FC
    Oktoba 8, 2018
    Azam v Coastal Union 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JUMA ABDUL, AKILIMALI WAREJEA KUIONGEZEA NGUVU YANGA MECHI NA MBAO FC JUMAPILI TAIFA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top