Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Ndugu Wallace Karia ametuma salamu za rambirambi kwa aliyekuwa mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Rajabu Digongwa aliyefariki mkoani Tanga.
Karia amesema kwamba amepokea kwa huzuni na mshituko mkubwa taarifa za kifo cha mchezaji huyo wa zamani aliyefariki dunai jana baada ya kuugua.
Karia ametoa pole kwa familia ya mchezaji huyo, wanafamilia wa mpira wa miguu, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu.
“Marehemu Digongwa namfahamu vizuri toka enzi akicheza na kifo chake kimenishitua na kunihuzunisha, kwa niaba ya TFF natoa pole kwa wafiwa" alisema Karia.
Mshambuliaji wa zamani wa Pamba ya Mwanza, Khalid Bitebo 'Zembwela' amefiwa na mkewe
Enzi za uhai wake marehemu Digongwa alicheza timu za Wananchi FC, African Sports, pia alipata kuitwa kwenye timu ya mkoa wa Tanga na pia timu ya Taifa ya Tanzania.
Mazishi ya marehemu Digongwa yamefanyika leo majira ya saa 4 asubuhi mkoani Tanga
Wakati huo huo: Rais Karia pia ametuma salamu za rambirambi kwa mshambuliaji wa zamani wa Pamba ya Mwanza, Khalid Bitebo 'Zembwela' aliyefiwa na mkewe.
Ametoa pole kwa Bitebo na familia kiujumla akiwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha majonzi.
RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Ndugu Wallace Karia ametuma salamu za rambirambi kwa aliyekuwa mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Rajabu Digongwa aliyefariki mkoani Tanga.
Karia amesema kwamba amepokea kwa huzuni na mshituko mkubwa taarifa za kifo cha mchezaji huyo wa zamani aliyefariki dunai jana baada ya kuugua.
Karia ametoa pole kwa familia ya mchezaji huyo, wanafamilia wa mpira wa miguu, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu.
“Marehemu Digongwa namfahamu vizuri toka enzi akicheza na kifo chake kimenishitua na kunihuzunisha, kwa niaba ya TFF natoa pole kwa wafiwa" alisema Karia.
Mshambuliaji wa zamani wa Pamba ya Mwanza, Khalid Bitebo 'Zembwela' amefiwa na mkewe
Enzi za uhai wake marehemu Digongwa alicheza timu za Wananchi FC, African Sports, pia alipata kuitwa kwenye timu ya mkoa wa Tanga na pia timu ya Taifa ya Tanzania.
Mazishi ya marehemu Digongwa yamefanyika leo majira ya saa 4 asubuhi mkoani Tanga
Wakati huo huo: Rais Karia pia ametuma salamu za rambirambi kwa mshambuliaji wa zamani wa Pamba ya Mwanza, Khalid Bitebo 'Zembwela' aliyefiwa na mkewe.
Ametoa pole kwa Bitebo na familia kiujumla akiwataka kuwa na subira katika kipindi hiki cha majonzi.
0 comments:
Post a Comment