Pep Guardiola amethibitisha kwamba Yaya Toure ataondoka baada ya msimu huu Manchester City PICHA ZAIDI GONGA HAPA
KIUNGO Yaya Toure tayari ameanza kupiga hesabu za maisha nje ya Manchester City na anatazamiwa kubaki Ligi Kuu ya England baada ya kuambiwa hatapewa mkataba mpya Etihad.
Pep Guardiola amethibitisha Ijumaa kwamba Muivory Coast huyo atahitimisha miaka yake nane ndani ya klabu hiyo, lakini inaaminika Toure anataka kuendelea kucheza England.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 anatarajiwa kupewa Unahodha katika mchezo wake wa mwisho dhidi ya Brighton Jumatano na atakabidhiwa zawadi baada ya mechi kuutambua mchango wake katika klabu hiyo.
Guardiola pia amesema mchezo dhidi ya Brighton utakuwa maalum wa Toure kuwaaga mashabiki Uwanja wa Etihad.
"Hatabaki msimu huu,"amesema Guardiola.
0 comments:
Post a Comment