Mshambuliaji wa Barcelona, Luis Suarez (kushoto) akiwekeana mkwara na Sergio Ramos wa Real Madrid (kulia) wakati wa mechi ya La Liga baina ya mahasimu hao wa Hispania, maarufu kama El Clasico timu hizo zikitoa sare ya 2-2 usiku wa Jumapili. Mabao ya Barca iliyomaliza pungufu baada ya Sergi Roberto kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 45 na ushei yalifungwa na Luis Suarez dakika ya 10 na Lionel Messi dakika ya 52, wakati ya Real yalifungwa na Cristiano Ronaldo dakika ya14 na Gareth Bale dakika ya 72. Ronaldo alitolewa anachechemea na nafasi yake kuchukuliwa na Marco Asensio dakika ya 46 baada ya kuumia enka PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Man who fatally shot ex-Saints star Will Smith after 2016 car crash gets 25
years in jail
-
Cardell Hayes, 36, was convicted of manslaughter in Dec. 2016 but the jury
vote had been 10-2 and the conviction was later tossed after the US Supreme
Cour...
20 minutes ago
0 comments:
Post a Comment