BONDIA Anthony Joshua amefungua milango kwa ya pambano kubwa la ngumi za kulipwa uzito wa juu duniani na David Haye, ikiwa Hayemaker atashinda pambano la marudiano na Tony Bellew usiku wa Jumamosi.
Mbabe huyo anayeshikilia mataji yote ya uzito wa juu duniani kasoro moja tu, yupo kwa majadiliano ya ofa ya dola za Kimarekani Milioni 50 kupigana na bingwa wa WBC, Deontay Wilder, lakini atakuwa tayari kupigana na Haye kwanza kama dili hilo litaendelea kusuasua.
Haye amemjibu Joshua kwa kusema: "Anaweza kupata hiyo kazi na mimi. Ikiwa yeye au Wilder wako siriasi wanaweza kupata hilo pambano, hakuna tatizo,".
0 comments:
Post a Comment