• HABARI MPYA

    Thursday, March 15, 2018

    PAKA AKATIZA UWANJANI NA KUSIMAMISHA MECHI BAYERN IKISHINDA 3-1

    Paka akipanda mabango ya pembezoni mwa Uwanja kuondoka uwanjani baada ya kuvamia ghafla na kusababisha mchezo wa marudiano hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya baina ya wenyeji, Besiktas na Bayern Munich ya Ujerumani kusimama kwa muda Uwanja wa Vodafone mjini İstanbul, Uturuki kipindi cha pili.
    Bayern Munich ilishinda 3-1 mabao yake yakifungwa na Thiago Alcantara dakika ya 18, Gokhan Gonul aliyejifunga dakika ya 46 na Sandro Wagner dakika ya 84, huku la Besiktas likifungwa na Vagner Love dakika ya 59 na sasa mabingwa wa Ujerumani wanasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 8-1 baada ya kushinda 5-0 kwenye mchezo wa kwanza nyumbani PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: PAKA AKATIZA UWANJANI NA KUSIMAMISHA MECHI BAYERN IKISHINDA 3-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top