• HABARI MPYA

    Wednesday, January 17, 2018

    MKHITARYAN NJIA MOJA KUEKELEA ARSENAL KUMPISHA SANCHEZ UNITED

    KIUNGO Henrikh Mkhitaryan anatarajiwa kujiunga na Arsenal kutoka Manchester United licha ya onyo kutoka kwa wakala wake kwamba anaweza kuvuruga usajili wa Alexis Sanchez kwenda Old Trafford.
    Uhamisho wa Mkhitaryan kwenda Emirates unakaribia baada ya kugundulika United wameipiku Manchester City katika mbio za kuwania saini ya Sanchez kutoka Arsenal.
    Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Armenia mkataba wake Old Trafford unamalizika mwaka 2020 na wakala wake, Mino Raiola amesema anaweza kuondoka kwa vipengele vyake binafasi au kubadilishwa na Sanchez.
    Pamoja na hayo inafahamika kwamba Mkhitaryan amekubali hana maisha zaidi United na sasa anatarajia majadiliano ya kuongeza mshahara wake kutoka Pauni 140,000 kwa wiki anazolipwa sasa.

    Kiungo wa Manchester United, Henrikh Mkhitaryan anatarajiwa kujiunga na Arsenal PICHA ZAIDI GONGA HAPA  

    Raiola, ambaye aliingiza Pauni Milioni 41 katika mauzo ya Paul Pogba ya Pauni Milioni 89 kwenda United kutoka Juventus na pia alimuwakilisha Zlatan Ibrahimovic, pia anaweza kuwa sehemu ya dili hili.
    Arsenal wanataka Pauni Milioni 35 kumuuza Sanchez ambaye atakuwa anapata mshahara wa Pauni 350,000 kwa wiki United pamoja na Pauni Milioni 20 za kusaini mkataba na Pauni Milioni 15 atakazolipwa wakala wake, Fernando Felicevich.
    Mkhitaryan alijiunga na United kwa dau la Pauni Milioni 26 kutoka Borussia Dortmund mwaka 2016 na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka ya 28 hakujumuishwa kwenye kikosi cha timu hiyo kilichomenyana na Stoke City usiku wa Jumatatu huku kocha Jose Mourinho akiweka wazi kwamba hana nafasi kwa sasa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MKHITARYAN NJIA MOJA KUEKELEA ARSENAL KUMPISHA SANCHEZ UNITED Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top