Kocha Jose Mourinho wa Manchester United amepangiwa Yeovil katika raundi ya Nne ya kombe la FA England PICHA ZADII GONGA HAPA
TIMU ya Manchester United imepangwa na timu ya kiwango cha chini katika Raundi ya Nne ya Kombe la FA, Yeovil Town ya Daraja la Pili, mechi ambayo itachezwa kabla ya mchezo wa kiporo wa Raundi ya Tatu kati ya Brighton na Crystal Palace Uwanja wa AMEX.
The Glovers, waliyoitoa Bradford kwenye raundi iliyopita wamejikuta wanaangukia kwa timu ya kocha Jose Mourinho Raundi hii.
Yeovil watawakaribisha vigogo wa England, walioitoa Derby kwenye raundi iliyopita Uwanja wa mashabiki 9,665 wa Huish Park mwishoni mwa mwezi uliopita.
Tottenham imepangwa na timu ya Daraja la Pili pia na watasafiri kwenda Rodney Parade kucheza na Newport.
Kikosi cha Mike Flynn kiliwafunga Leeds katika mechi ya aina yake ya Raundi ya Tatu iliyoshuhudiwa Shawn McCoulsky akiifungia bao la ushindi dakkika ya 89 klabu Wales na kuisogeza mbele.
Washindi mara saba, Liverpool wamepangiwa West Brom katika mechi nyingine ya timu za Ligi Kuu tupu.
Chelsea inaweza kukutana na Newcastle, lakini kikosi cha Antonio Conte kwanza lazima kiwatoe Norwich — katika mechi ya marudio baada ya kulazimishwa sare Uwanja wa Carrow Road wikiendi iliyopita.
Bournemouth nao wanaweza kukutana na West Ham katika mechi ya timu za Ligi Kuu tupu, lakini lazima timu zote zishinde dhidi ya Wigan na Shrewsbury.
Vinara wa Ligi Kuu, Manchester City wanakabiliwa na safari ya aidha Cardiff au Mansfield na Leicester lazima wafuzu katika mechi ya marudio Fleetwood ili wakamenyana na Peterborough Uwanja wa ABAX.
Nottingham Forest, waliowatoa mabingwa wa sasa, Arsenal kwa mabao 4-2 Uwanja wa City Jumapili iliyopita, itasafiri kuwafuata wababe wa Championship, Hull baada ya mafanikio hayo.
Mechi zote za za Raundi ya nne zitachezwa wikiendi ya Januari 26 na 29.
0 comments:
Post a Comment