• HABARI MPYA

    Sunday, January 07, 2018

    ARSENAL WATEMESHWA UBINGWA WA FA NA 'TIMU YA MCHANGANI'

    Wachezaji wa Arsenal wakierejea katikati kinyonge kuanzisha mpira baada ya kufungwa bao la tatu katika kipigo cha 4-2 mbele ya wenyeji, Nottingham Forest katika mchezo wa Raundi ya Tatu ya Kombe la FA leo Uwanja wa The City Ground mjini Nottingham, Nottinghamshire. Arsenal waliokuwa mabingwa watetezi wanavuliwa ubingwa na kutolewa na timu hiyo ya Daraja la Kwanza, Championship. Mabao ya Nottingham yamefungwa na Eric Lichaj mawili dakika ya 20 na 44, Ben Brereton kwa penalti dakika ya 64 na Kieran Dowell kwa penalti pia dakika ya 85, wakati ya Arsenal yamefungwa na Per Mertesacker dakika ya 23 na Danny Welbeck dakika ya 79 PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL WATEMESHWA UBINGWA WA FA NA 'TIMU YA MCHANGANI' Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top