• HABARI MPYA

    Wednesday, December 13, 2017

    SIMBA KUANZIA DJIBOUTI KOMBE LA SHIRIKISHO

    Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
    SIMBA SC itaanza na Gendarmerie Tnale ya Djibouti katika Raundi ya Awali ya Kombe la Shirikisho Afrika mwakani, mechi ya kwanza ikichezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na marudiano ugenini.
    Mashirikisho ya nchi nane tu hayajawasilisha wawakilishi ambayo ni ya Cape Verde, Chad, Eritrea, Namibia, Reunion, Sao Tome and Principe, Sierra Leone na Somalia.
    Ikivuka hatua hiyo, Ikivuka hapo, Simba itakutana na mshindi kati ya El Masry ya Misri na Green Bufaloes ya Zambia.

    Simba itaanza na Gendarmerie Tnale ya Djibouti katika Raundi ya Awali ya Kombe la Shirikisho Afrika 

    Katika michuano hiyo pia kuna timu za USM Alger ya Algeria, Zamalek ya Misri, Raja Casablanca ya Morocco, Enyimba ya Nigeria, DC Motema Pembe ya DRC, SuperSport United ya Afrika Kusini, Al Ahly Shandy na Al Hilal Obied za Sudan, Club Africain ya Tunisia na Nkana FC ya Zambia. RATIBA KAMILI GONGA HAPA
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA KUANZIA DJIBOUTI KOMBE LA SHIRIKISHO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top