• HABARI MPYA

    Thursday, December 07, 2017

    RONALDO AFUNGA REAL MADRID YAIPIGA 3-2 BORUSSIA DORTMUND

    Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo akinyoosha mkono juu na kuinua kidole gumba kuwapa ishara mashabiki wa timu yake baada ya kufunga bao la pili dakika ya 12 katika ushindi wa 3-2 dhidi ya Borussia Dortmund kwenye mchezo wa Kundi H Ligi ya Mabingwa usiku wa jana Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid, Hispania. Mabao mengine ya Real Madrid yalifungwa na Borja Mayoral dakika ya nane na Lucas Vázquez dakika ya 81 wakati ya Borussia Dortmund yote yalifungwa na  Pierre-Emerick Aubameyang dakika za 43 na 48. Real inakwenda 16 Bora kama mshindi wa pili wa kundi baada ya kumaliza na pointi 13, nyuma ya Tottenham Hotspur iliyomaliza na pointi 16, wakati Borussia Dortmund inaangukia Europa League baada ya kumaliza nafasi ya tatu PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO AFUNGA REAL MADRID YAIPIGA 3-2 BORUSSIA DORTMUND Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top