• HABARI MPYA

    Friday, December 08, 2017

    LOOKMAN AIFUNGIA MAWILI EVERTON YASHINDA 3-0 ULAYA

    Ademola Lookman akishangilia na chipukizi wenzake, Fraser Hornby (kushoto) na Harry Charsley baada ya kufunga mabao mawili dakika za 21 na 28 katika ushindi wa 3-0 wa Everton dhidi ya wenyeji, Apollon kwenye mchezo wa Kundi E Europa League usiku wa Alhamisi Uwanja wa Neo GSP mjini Nicosia, Cyprus. Bao lingine la Everton ambayo ilikwenda kwenye mechi hiyo bila kocha wake mpya, Sam Allardyce lilifungwa na Nicola Vlasic dakika ya 87, lakini pamoja na ushindi huo safari yao inaishia hapo baada ya kumaliza nafasi ya tatu kwa pionti zao nne nyuma ya Atalanta iliyomaliza kileleni klwa pointi zake 14 na Olympique Lyonnais pointi 11 PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LOOKMAN AIFUNGIA MAWILI EVERTON YASHINDA 3-0 ULAYA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top