• HABARI MPYA

    Monday, November 20, 2017

    HAYE AUMIA, PAMBANO LAKE NA BELLEW LAAHIRISHWA TENA

    BONDIA David Haye amelazimika kuahirisha pambano lake na Tony Bellew baada ya kuumia mkono kufuatia kuanguka kwenye ngazi.
    Wawili hao walitarajiwa kuwa na pambano la marudiano Desemba 17 ukumbi wa O2 mjini London baada ya Bellew kumsimamisha raundi ya 11 mwezi Machi.
    Katika pambano hilo, Haye aliumia raundi za mwanzoni na ikamsababisha kupoteza pambano hilo.
    Na akiwa kwenye maandalizi ya pambano la marudiano, bondia huyo mwenye umri wa miaka 37 ameumia tena na sasa pambano linaahirishwa tena hadi Machi 24 au Mei 5.

    David Haye amelazimika kuahirisha pambano lake na Tony Bellew baada ya kuumia mkono
     PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: HAYE AUMIA, PAMBANO LAKE NA BELLEW LAAHIRISHWA TENA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top