• HABARI MPYA

    Tuesday, November 14, 2017

    BAKAYOKO ASEMA N'GOLO KANTE IS 'SI MZURI’ KULIKO YEYE

    London, ENGLAND
    KIUNGO wa Chelsea, Tiemoue Bakayoko amesema mchezaji mwenzake na mshindi wa tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwaka wa PFA, N'Golo Kante is 'si mzuri' kuliko yeye. 
    Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 hakuitwa kwenye kikosi cha kocha Didier Deschamps cha Ufaransa kwa ajili ya mechi za kirafiki za kimataifa wiki iliyopita na pia hakujumuishwa kwenye kikosi kilichocheza mechi za kufuzu Kombe la Dunia Oktoba.
    Bakayoko amesema anaheshimu uamuzi wa kocha Deschamps, lakini naye ni mzuri ukilinganisha na wachezaji wanaoteuliwa badala yake. 

    Tiemoue Bakayoko amesema N'Golo Kante 'si mzuri' kuliko yeye PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    “Inanisikitisha,”amesema Bakayoko. “Naamini bado ni malengo yangu kucheza kwenye hili Kombe la Dunia. Ninacheza katika klabu kubwa, nafikiri inaweza kunisaidia,”.
    “Nafikiri [Adrien] Rabiot, Kante, [Blaise] Matuidi, [Corentin] Tolisso si wazuri kuliko mimi. Naheshimu uchaguzi wa kocha na pia ninawaheshimu wachezaji walioteuliwa, waa vipaji, ni marafiki,”. “Ninajivunia kwamba wanateuliwa, Ningependa kuwa nao. Lakini si mbaya kuliko wao.”alisema.
    Bakayoko amecheza mechi 15 klabu ya Chelsea tangu ajiunge nayo msimu huu ambaye kocha Antonio Conte alimsajili kuziba pengo la Nemanja Matic aliyehamia Manchester United.
    Mfaransa huyo alifunga mabao mawili katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Qarabag kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya na akafunga pia timu ikichapwa 2-1na Crystal Palace.
    Kante ameshinda mataji ya Ligi Kuu ya England misimu miwili mfululizo iliyopita kwa misimunmiwili iliyopita, kwnza akiwa na Leicesterna baadat na Chelsea. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BAKAYOKO ASEMA N'GOLO KANTE IS 'SI MZURI’ KULIKO YEYE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top