• HABARI MPYA

    Monday, October 16, 2017

    KAKA AMWAGA MACHOZI AKICHEZA MECHI YA MWISHO MAREKANI

    Mwanasoka bora wa zamani wa dunia, Ricardo Izecson dos Santos 'Kaka' akibubujikwa machozi jana kabla ya mchezo wa mwisho kuichezea timu yake, Orlando City ikifungwa 1-0 na Columbus Crew katika Ligi ya Marekani, maarufu kama MLS Uwanja wa Orlando City mjini Orlando, Florida. Kaka anaondoka Orlando baada ya kuifungia mabao 24 katika mechi 73 tangu mwaka 2014 alipojiunga nayo akitokea AC Milan, baada ya kuzichezea Sao Paulo ya kwao, Brazil na Real Madrid ya Hispania, lakini hajasema kama anastaafu moja kwa moja au atakwenda kuendelea kucheza sehemu nyingine PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAKA AMWAGA MACHOZI AKICHEZA MECHI YA MWISHO MAREKANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top