• HABARI MPYA

    Wednesday, September 06, 2017

    SIMBA MAZOEZINI LEO UWANJA WA UHURU KUJIANDAA NA AZAM

    Mshambuliaji wa Simba, John Bocco akiondoka na mpira mazoezini leo Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam kujiandaa na mchezo ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya timu yake ya zamani, Azam FC Jumamosi Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam
    Mshambuliaji Mrundi, Laudit Mavugo akipiga mpira mbele ya wenzake leo mazoezini Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam
    Beki Salim Mbonde akipiga mpira mbele ya wenzake leo mazoezini Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam 
    Nyota wa Simba wakipigiana pasi leo mazoezini Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam 

    Wachezaji wa Simba wakiwa mazoezini Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam leo 
    Simba imehamishia mazoezi yake Uwanja wa Uhuru nyasi bandia kutoka Boko Veterani kwa kuwa Azam Complex ni wa nyasi bandia pia
    Hapa wachezaji wa Simba wakifanya dua baada ya mazoezi yao 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA MAZOEZINI LEO UWANJA WA UHURU KUJIANDAA NA AZAM Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top