• HABARI MPYA

    Sunday, September 10, 2017

    SAMATTA AGONGA DAKIKA 90 GENK YAPATA SARE GENT, 1-1

    Na Mwandishi Wetu, GENT
    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta leo amecheza kwa dakika zote 90, timu yake, KRC Genk ikilazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na AA Gent katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A, Ubelgiji Uwanja wa Ghelamco-Arena mjini Gent.
    Samatta alicheza vizuri mchezo huo mgumu wa ugenini leo, akisaidia ulinzi na pia kutekeleza wajibu wake kama mshambuliaji.
    Na kulikuwa kuna mchango wake pia katika bao la timu yake, Genk lililofungwa na beki kutoka Jamhuri ya Czech, Jakub Brabec aliyemalizia pasi ya kiungo Mspaniola, Alejandro Pozuelo dakika ya 89 baada ya Gent kutangulia kwa bao la penalti la kiungo Mswisi, Danijel Milicevic dakika ya 35.
    Mbwana Samatta akitafuta maarifa ya kumpita beki wa Gent leo
    Huo unakuwa mchezo wa 61 kwa Samatta katika mashindano tangu Januari mwaka jana alipojiunga na Genk, kati ya hiyo mechi 36 alianza na mechi 22 ametokea benchi.
    Katika mechi hizo, mshambuliaji huyo wa zamani wa African Lyon, zamani Mbagala Market na Simba zote za Dar e Salaam, amefunga jumla ya mabao 21. 
    Kikosi cha AA Gent kilikuwa: Kalinic, Gigot, Dussenne, Machado, Asare, Marcq, Esiti, Dejaegere/Andrijasevic dk85, Milicevic/Bronn dk45, Sylla na Simon/Kubo dk73..
    KRC Genk: Vukovic, Mata/Maehle dk45, Brabec, Colley, Uronen, Berge, Malinovskyi/Zhegrova dk80, Pozuelo, Samatta, Writers na Ingvartsen/Heynen dk93.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SAMATTA AGONGA DAKIKA 90 GENK YAPATA SARE GENT, 1-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top