• HABARI MPYA

    Saturday, September 02, 2017

    MECHI YA SIMBA NA AZAM YASOGEZWA MBELE SABABU YA OKWI

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) kesho linatarajiwa kutoa ratiba mpya ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara iliyofanyiwa marekebisho na ndani yake mchezo kati ya Azam FC na Simba SC uliokuwa ufanyike Septemba 6 umesogezwa mbele hadi Septemba 9.
    Na hatua hiyo inafuatia maombi ya klabu ya Simba kutaka mchezo huo usogezwe mbele kwa kuwa wachezaji wake wawili tegemeo, beki Juuko Murshid na mshambuliaji Emmanuel Okwi hawatakuwepo.
    Emmanuel Okwi amekuwa sababu ya kuahirishwa kwa mchezo kati ya Azam na Simba
    Wawili hao wapo na timu yao ya taifa, Uganda ambayo inajiandaa kwa mchezo wa Kundi E kufuzu Kombe la Dunia mwakani Urusi dhidi ya wenyeji, Misri Septemba 5. Mchezo wa kwanza baina ya timu hizo, Agosti 31 Uganda walishinda 1-0 mjini Kampala.
    Hata Uganda wakiondoka Cairo siku moja tu baada ya mchezo hakuna namna Juuko na Okwi wanaweza kuwahi mechi na Azam jioni ya Septemba 6, hivyo TFF imeusogeza mbele mchezo huo hadi Septemba 9.
    Na TFF imeiagiza Bodi ya Ligi kuhakikisha haipangi mechi wakati wa ratiba za michezo ya kimataifa, kuepuka mambo kama ambayo yanasababisha mechi ya Azam na Simba kusogezwa mbele.Nicholas Gyan ataondoka kurejea klabu yake, Ebusua Dwarfs ya kwao, Ghana ili kukamilisha taratibu za uhamisho wake.
    Akizungumza na Bin Zubeiry Sports – Online leo, Hans Poppe amesema kwamba, Gyan alilazimika kuja kushiriki tamasha la Simba Day ambalo ni maalum kwa utambulisho wa wachezaji wapya, lakini leo anarejea Ghana.
    Hans Poppe amesema kwamba Gyan anamaliza mkataba wake Agosti 20, mwaka huu Ebusua Dwarfs na baada ya hapo atarejea nchini – maana yake anaweza kuiwahi mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya mahasimu, Yanga Agosti 23, mwaka huu.
    Wakati huo huo: Mshambuliaji mpya, Nicholas Gyan amerejea leo asubuhi Dar es Salaam tayari kuanza rasmi maisha mapya katika klabu yake mpya aliyojiunga nayo mwezi uliopita kutoka Ebusua Dwarfs ya kwao, Ghana.
    Gyan aliondoka nchini Agosti 9 baada ya kutambulishwa Simba SC katika tamasha la Simba Day Uwanja wa Taifa kurejea Ghana kukamilisha taratibu za uhamisho wake na baada ya kufanikisha hilo, tayari yupo nchini.
    Wachezaji wengine wa kigeni Simba SC kiungo Mghana, James Kotei, beki Mzimbabwe na Nahodha Method Mwanjali, kiungo Mnyarwanda, Haruna Niyonzima na mshambuliji Mrundi, Laudit Mavugo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MECHI YA SIMBA NA AZAM YASOGEZWA MBELE SABABU YA OKWI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top