• HABARI MPYA

    Tuesday, August 15, 2017

    UCHAGUZI BODI YA LIGI KUFANYIKA JUMAPILI DAR

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    Uchaguzi wa Kamati ya Uongozi (Management Committee) ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara utafanyika Jumapili Oktoba 15, 2017 jijini Dar es Salaam.
    Fomu kwa ajili ya wagombea zitaanza kutolewa Agosti 17, 2017 kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu kwa wagombea ni saa 10.00 jioni Agosti 23, mwaka huu.
    Nafasi zitakazowaniwa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Wajumbe watatu kuwakilisha klabu za Ligi (PL), Wajumbe wawili wa kuwakilisha klabu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL), na Mjumbe mmoja wa kuwakilisha klabu za Ligi Daraja la Pili (SDL).
    Ada ya fomu kwa nafasi za Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti ni Sh 200,000 (Shilingi lakini mbili) wakati nafasi nyingine zilizobaki ni Sh 100,000 (Shilingi laki moja).
    Uchaguzi utaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za Uchaguzi za TFF toleo la 2013.
    Wagombea kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji wa Bodi ya Ligi Kuu ni marais au wenyeviti wa klabu husika.
    Wagombea wanatakiwa kuwa wenyeviti au Marais wa klabu husika.
    Nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania inagombewa na klabu za Ligi Kuu pekee.
    Wakati huo huo: Viongozi wa Klabu zinazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza (FDL), wanatarajiwa kuwa na kikao na uongozi wa Bodi ya Ligi (TPLB), kitakachofanyika Ijumaa Agosti 8, 2017 kuanzia saa 3.00 asubuhi kwenye Hosteli za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).
    Pamoja na mambo mengine, kikao hicho kitakuwa maalumu kwa ajili ya kujadili Ligi Daraja la Kwanza lakini pia kutoa semina kwa viongozi hao kuhusu Leseni za Klabu (Club License).
    TFF inatoa wito kwa viongozi wa juu wa klabu kuhudhuria kikao hicho muhimu . TFF ingependa kusisitiza kuzingatia muda wa kuanza kikao.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: UCHAGUZI BODI YA LIGI KUFANYIKA JUMAPILI DAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top