Mshambuliaji Mbrazil, Neymar akiwa amempanda mgongoni mchezaji mwenzake, Edinson Cavani kufurahia baada ya wote kufunga katika ushindi wa Paris Saint-Germain wa 3-0 dhidi ya wenyeji Guingamp 3-0 kwenye mchezo wa Ligue 1 Ufaransa jana Uwanja wa Roudourou mjini Guingamp. Neymar alitoa pasi ya bao pili lililofungwa na Cavani dakika ya 62, kabla ya yeye mwenye kufunga bao lake la kwanza PSG dakika ya 82 katika mechi hiyo ya kwanza kwake baada ya kusajiliwa kwa dau la rekodi ya dunia Pauni 198 kutoka Barcelona ya Hispania, huku beki Mkongo, Jordan Ikoko akijifunga dakika ya 52 kuwapa bao la kwanza wapinzani PICHA ZAIDI GONGA HAPA
Nic Claxton Contract a 'Priority' in 2024 NBA Free Agency, Nets HC
Fernández Says
-
Newly installed Brooklyn Nets head coach Jordi Fernández made it abundantly
clear he considers fifth-year center Nic Claxton to be a big part of the…
27 minutes ago
0 comments:
Post a Comment