• HABARI MPYA

    Monday, August 14, 2017

    KLOPP AWATEMA COUTINHO NA STURRIDGE SAFARIYA UJERUMANI

    KIKOSI CHA LIVERPOOL KILICHOSAFIRI LEO

    Trent Alexander-Arnold, Alberto Moreno, Dejan Lovren, James Milner, Georgio Wijnaldum, Jordan Henderson, Emre Can, Sadio Mane, Mohamed Salah, Roberto Firmino, Ryan Kent, Dominic Solanke, Divock Origi, Joe Gomez, Ragnar Klavan, Jon Flanagan, Andy Robertson, Joel Matip, Marko Grujic, Simon Mignolet, Loris Karius na Danny Ward. 


    Kocha Jurgen Klopp amekiongoza kikosi cha Liverpoool kwa safari ya Ujerumani leo bila Philippe Coutinho na Daniel Sturridge kwa ajili ya mchezo dhidi ya Hoffenheim kesho.  
    PICHA ZAIDI GONGA HAPA


    TIMU ya Liverpool imeondoka leo na kikosi cha wachezaji 22 kwenda Ujerumani bila Philippe Coutinho na Daniel Sturridge kwa ajili ya mchezo fwa kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Hoffenheim. 
    Kocha Mjerumani, Jurgen Klopp na Jordan Henderson walikiogoza kikosi hicho Uwanja wa Ndege wa Liverpool leo wakati wanajiandaa kuondoka kwa ajili ya mchezo wa kwanza wa hatua ya mchujo kesho Kusini Magharibi mwa Ujerumani kabla ya timu hizo kurudiana Jijini Anfield Jumatano ijayo.
    Coutinho aliukosa mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya England wa Liverpool ikitoa sare ya 3-3- na wenyeji, Watford kutokana na maumivu ya mgongo, lakini awali ikachukuliwa kama analazimisha uhamisho wa kwenda Barcelona.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KLOPP AWATEMA COUTINHO NA STURRIDGE SAFARIYA UJERUMANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top