BEKI wa kati Per Mertesacker anatarajiwa kupewa jukumu la ukocha wa akademi Arsenal kuanzia msimu ujao, ingawa hajatangaza kustaafu.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani, ataendelea kuwa sehemu ya kikosi cha kwanza cha Arsene Wenger msimu ujao, lakini amepanga kupanua uelewa wake juu ya soka na kuanza kujipanga kwa kazi yake baadaye atakapostaafu.
Wenger anavutiwa mno na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, Mertesacker ambaye anaamini anafaa mno kwa kazi hiyo.
Per Mertesacker anatarajiwa kupewa ukocha wa akademi ya Arsenal kuanzia msimu ujao PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment