Kiungo wa Manchester United, Michael Carrick akitabasamu katika mazoezi ya kwanza kama Nahodha wa timu PICHA ZAIDI GONGA HAPA
KLABU ya Manchester United imemthibitisha Michael Carrick kuwa Nahodha mpya, baada ya Wayne Rooney kuondoka.
Rooney ameondoka Manchester kurejea Everton baada ya miaka 13 na sasa Carrick anakuwa Nahodha mpya.
Kikosi cha Mashetani hao Wekundu kwa sasa kipo mjini Los Angeles, Marekani na nyota wake mbalimbali, akiwemo mshambuliaji mpya, Romelu Lukaku kutoka Everton na kiungo nyota, Paul Pogba kwa maandalizi ya msimu mpya.
Nyota hao wa Old Trafford leo wamefanya mazoezi kwenye jua angavu la asubuhi viwanja vya mazodezi vya UCLA katika ziara yao ya Marekani.
Lukaku alichangamsha mazoezi hayo ya awali akipigwa picha amewabeba wote, Paul Pogba na Jess Lingard uwanjan. Hayo yalikuwa mazoezi ya pili kwa Mbelgiji na wachezaji wenzake wapya, baada ya kusajiliwa kwa dau la Pauni Milioni 75 kutoka Everton.
Hata kocha Jose Mourinho akajikuta anatabasamu wakati akiwaagalia nyota wake walivyoanza mazoezi kufuatia mapumziko ya baada ya msimu. Lakini muda mrefu kazi halisi itaanza kwa kuanza na mechi nne wiki ijayo.
Mashetani hao Wekundu watacheza na LA Galaxy na Real Salt Lake City kabla ya kumenyana na vigogo wenzao wa Ulaya, Manchester City na Real Madrid na kurejea Manchester.
Kisha watacheza mechi mbili zaidi upande mwingine wa Atlantic, wakimenyana na Valerenga mjini Oslo kabla ya kumaliza na Sampdoria mjini Dublin.
0 comments:
Post a Comment