TIMU ya Zesco United jana imepata ushindi wa 1-0 dhidi ya Recreativo Desportivo do Libolo katika mchezo wa Kundi C Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Levy Mwanawasa mjini Ndola, Zambia.
Katika mchezo huo, timu zote zilimaliza pungufu, Libolo wakimpoteza Celson Costa na Zesco wakimpoteza Anthony Akum baada ya wote kuonyeshwa kadi za pili za njano na kutilewa kwa kadi nyekundu dakika za 86 na 87.
Baada ya kuonyeshwa kadi za njano kwa rafu za mapema kwenye mchezo huo, Costa kwa kumchezea rafu Dave Daka kwenye eneo la penalti la Libolo na Akum kwa kumchezea rafu Julsy Kaya na refa wa Namibia, Jackson Pavaza hakusita kuwatoa nje kwa kadi za pili za njano zikiwa zimebaki dakika tatu mchezo kumalizika.
Bao pekee la washindi lilipatikana dakika ya 26 katika mchezo hup, mfungaji Idriss Mbombo aliyemalizia krosi ya Dave Daka na sasa Zesco United wanaongoza Kundi C baada ya Smouha na El Hilal El Obeid kutoka sare ya 1-1.
Sasa wana pointi sita baada ya kucheza mechi tatu, wakati Smouha ni ya pili ikiwa na pointi nne ikitofautiana tu kwa wastani wa mabao na El Hilal El Obeid katika nafasi ya tatu na Recreativo Desportivo do Libolo inashika mkia kwa pointi zake tatu.
Mechi zijazo za kundi hilo zitachezwa Juni 20, wakati Zesco United itakaposafiri kuifuata Clube Recreativo Desportivo do Libolo na El Hilal El Obeid watawakaribisha Smouha.
MATOKEO YOTE KOMBE LA SHIRIKISHO;
Juni 4, 2017
CS Sfaxien 3 - 0 Platinum Stars
TP Mazembe 2 - 2 Supersport United
ZESCO United 1 - 0 Recreativo do Libolo
Juni 3, 2017
Smouha SC 1 - 1 Al Hilal Al Ubayyid
CF Mounana 0 - 1 Horoya
KCCA 2 - 1 Rivers United FC
FUS Rabat 2 - 1 Club Africain
Juni 2, 2017
Mbabane Swallows 0 - 0 MC Alger
Katika mchezo huo, timu zote zilimaliza pungufu, Libolo wakimpoteza Celson Costa na Zesco wakimpoteza Anthony Akum baada ya wote kuonyeshwa kadi za pili za njano na kutilewa kwa kadi nyekundu dakika za 86 na 87.
Baada ya kuonyeshwa kadi za njano kwa rafu za mapema kwenye mchezo huo, Costa kwa kumchezea rafu Dave Daka kwenye eneo la penalti la Libolo na Akum kwa kumchezea rafu Julsy Kaya na refa wa Namibia, Jackson Pavaza hakusita kuwatoa nje kwa kadi za pili za njano zikiwa zimebaki dakika tatu mchezo kumalizika.
Bao pekee la washindi lilipatikana dakika ya 26 katika mchezo hup, mfungaji Idriss Mbombo aliyemalizia krosi ya Dave Daka na sasa Zesco United wanaongoza Kundi C baada ya Smouha na El Hilal El Obeid kutoka sare ya 1-1.
Sasa wana pointi sita baada ya kucheza mechi tatu, wakati Smouha ni ya pili ikiwa na pointi nne ikitofautiana tu kwa wastani wa mabao na El Hilal El Obeid katika nafasi ya tatu na Recreativo Desportivo do Libolo inashika mkia kwa pointi zake tatu.
Mechi zijazo za kundi hilo zitachezwa Juni 20, wakati Zesco United itakaposafiri kuifuata Clube Recreativo Desportivo do Libolo na El Hilal El Obeid watawakaribisha Smouha.
MATOKEO YOTE KOMBE LA SHIRIKISHO;
Juni 4, 2017
CS Sfaxien 3 - 0 Platinum Stars
TP Mazembe 2 - 2 Supersport United
ZESCO United 1 - 0 Recreativo do Libolo
Juni 3, 2017
Smouha SC 1 - 1 Al Hilal Al Ubayyid
CF Mounana 0 - 1 Horoya
KCCA 2 - 1 Rivers United FC
FUS Rabat 2 - 1 Club Africain
Juni 2, 2017
Mbabane Swallows 0 - 0 MC Alger
0 comments:
Post a Comment