Mabingwa watetezi, Chelsea wataanza msimu mpya wa Ligi Kuu England kwa kumenyana na Burnley Agosti 12 GONGA HAPA KUTAZAMA RATIBA KAMILI
MABINGWA wa Ligi Kuu ya England, Chelsea wataanza kutetea taji lao kwa kumenyana na Burnley Uwanja wa Stamford Bridge, London Agosti 12.
Kikosi cha Antonio Conte kitafuatiwa na mchezo dhidi ya washindi wa pili wa msimu uliopita, Tottenham Uwanja wa Wembley katika marudio ya Nusu Fainali ya Kombe la FA msimu uliopita.
Kikosi cha Jose Mourinho cha Manchester United kitawakaribisha West Ham Uwanja wa Old Trafford katika mechi ya ufunguzi, wakati jirani zao, City watasafiri hadi Uwanja wa Amex kjuwafuata wageni, Brighton.
Arsene Wenger ataanza msimu mpya na Arsenal yake kwa kumenyana na Leicester City, wakati Liverpool itasafiri kuwafuata Watford katika mchezo wa kwanza wa Marco Silva kazini Vicarage Road.
Spurs itakwenda Uwanja wa St James' Park kwa mchezo wa ufunguzi dhidi ya Newcastle United, ambao mechi iliyopita ya Ligi Kuu walishinda 5-1 dhidi ya timu ya Mauriccio Pochettino.
Wageni wa Ligi Kuu, Huddersfield Town watawafuata Crystal Palace, na Newcastle watazuru Uwanja wa John Smith wiki moja baadaye kwa mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu nyumbani ndani ya miaka 45.
Southampton itamenyana na Swansea City Uwanja wa St Mary's wakati West Bromwich Albion wataikaribisha Bournemouth Uwanja wa The Hawthorns na Everton wataanzia nyumbani kwa Stoke City.
0 comments:
Post a Comment