• HABARI MPYA

    Monday, June 12, 2017

    KAMUSOKO ANG'ARA, MUSONA APIGA TATU ZIMBABWE YAUA 3-0

    MSHAMBULIAJI Knowledge Musona jana ameiongoza Zimbabwe kwa mara ya kwanza kama Nahodha na kufunga mabao yote matatu katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Liberia mjini Harare.
    Katika mechi hiyo ya Kundi G kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, kiungo wa Yanga ya Tanzania, Thabani Kamusoko alicheza vizuri na kutoa mchango kwenye ushindi huo.
    Ilikuwa ni siku ya furaha kwa Ghana pia baada ya kuichapa Ethiopia 5-0 katika mbio za Cameroon 2019.
    hat trick ya Musona inaipeleka Zimbabwe kileleni mwa Kundi G kwa tofauti ya wastani wa mabao na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambayo Jumamosi iliwafunga jirani zao, Kongo Brazzaville 3-1 mjini Kinshasa.
    Musona anayecheza Ubelgiji, anakuwa Nahodha wa kwanza wa Zimbabwe tangu Peter Ndlovu mwaka 2004 kufunga hat-trick timu ya taifa wakiichapa Liberia 3-0.
    Alifunga mabao hayo dakika za 24 baada ya kubaki na kipa Boison Wynney, dakika ya 50 akimalizia pasi ya Kudakwashe Mahachi na 63 baada ya kazi nzuri ya Kamusoko.
    Mabao ya Ghana yalifungwa na mkongwe Asamoah Gyan dakika ya 10, John Boye, Ebenezer Ofori na Raphael Dwamena mawili, huo ukiwa mwanzo mzuri kwa kocha Kwesi Appiah akipewa nafasi ya kufundisha Ghana kwa mara ya pili baada ya kutolewa Raundi ya kwanza kwenye Kombe la Dunia Brazil mwaka 2014.
    Ushindi huo unaipeleka Ghana kileleni mwa Kundi Kundi F kwa tofauti ya mabao na Sierra Leone, ambao waliifunga Kenya 2-1 jana.
    Knowledge Musona akiondoka na mpira baada ya kufunga mabao yote matatu Zimbabwe ikishinda 3-0 dhidi ya Liberia nyumbani

    MATOKEO YA MECHI ZOTE ZA MWANZO KUFUZU AFCON 2019
    Juni 12, 2017  
    Tunisia 1 - 0 Misri
    Juni 11, 2017  
    Algeria 1 - 0 Togo
    Cape Verde 0 - 1 Uganda
    Cape Verde 0 - 1 Uganda
    Ghana 5 - 0 Ethiopia
    Benin 1 - 0 Gambia
    Jamhuri ya Afrika ya Kati  2 - 1 Rwanda
    Zimbabwe 3 - 0 Liberia
    Senegal 3 - 0 Equatorial Guinea
    Juni 10, 20117  
    Mali 2 - 1 Gabon
    Burkina Faso 3 - 1 Angola
    Ivory Coast 2 - 3 Guinea
    DRC 3 - 1 Kongo
    Tanzania 1 - 1 Lesotho
    Sierra Leone 2 - 1 Kenya
    Guinea-Bissau 1 - 0 Namibia
    Nigeria 0 - 2  Afrika Kusini
    Niger 0 - 0 Swaziland
    Cameroon 1 - 0 Morocco
    Botswana 0 - 1 Mauritania
    Zambia 0 - 1 Msumbiji
    Burundi 3 - 0 Sudan Kusini
    Malawi 1 - 0 Comoro
    Libya 5 - 1 Shelisheli
    Sudan 1 - 3 Madagascar
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KAMUSOKO ANG'ARA, MUSONA APIGA TATU ZIMBABWE YAUA 3-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top