TIMU ya Al Ahly SC ya Misri jana imeichapa mabao 2-0 Wydad Athletic Club ya Morocco katika mchezo wa Kundi D Ligi ya Mabingwa Afrika uliofanyika Uwanja wa Borg El Arab mjini Alexandria, Misri.
Shukrani kwao wafungaji wa mabao hayo, Moamen Zakaria dakika ya 24 na Junior Ajayi dakika ya 79 na sasa Ahly inapanda kileleni mwa kundi hilo, ikifikisha pointi saba sawa na Zanaco ya Zambia, inayozidiwa wastani wa mabao na Wamisri hao.
Uwanja wa Addis Ababa, Ethiopia bao pekee la Saladin Said dakika ya 60 lilitosha kuwapa wenyeji, Saint George ushindi wa 1-0 dhidi ya AS Vita.
Etoile du Sahel juzi ilipunguzwa kasi katika Ligi ya Mabingwa baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Al Hilal Omdurman Uwanja wa Olimpiki mjini Sousse.
Pamoja na matokeo hayo, vigogo hao wa Tunisia wanabaki kileleni mwa Kundi A wakiongoza kwa pointi tatu zaidi kufuatia ushindi wa Ferroviario Beira nyumbani mjini Maputo.
Baada ya kipindi cha kwanza kigumu, Zied Boughattas akawafungia bao la kwanza washindi hao wa mwaka 2007 wa Ligi ya Mabingwa bao la kuongoza dakika ya 57.
Timu ya Sudan ikafanikiwa kucheza mechi ya 24 bila kupoteza kwenye mashindano yote, baada ya kusawazisha bao hilo dakika ya 80 kupitia kwa Mohamed Musa mjinii Sousse.
MATOKOE YOTE LIGI YA MABINGWA AFRIKA
Juni 4, 2017
Al Ahly SC 2 - 0 Wydad Athletic Club
Saint George 1 - 0 AS Vita Club
Juni 3, 2017
Etoile du Sahel 1 - 1 Al-Hilal
Zanaco FC 2 - 1 Coton Sport
Ferroviario Beira 1 - 0 Al Merrikh
Juni 2, 2017
Zamalek SC 1 - 1 USM Alger
Mamelodi Sundowns 1 - 2 Esperance
CAPS United 2 - 4 Al Ahli Tripoli
Shukrani kwao wafungaji wa mabao hayo, Moamen Zakaria dakika ya 24 na Junior Ajayi dakika ya 79 na sasa Ahly inapanda kileleni mwa kundi hilo, ikifikisha pointi saba sawa na Zanaco ya Zambia, inayozidiwa wastani wa mabao na Wamisri hao.
Uwanja wa Addis Ababa, Ethiopia bao pekee la Saladin Said dakika ya 60 lilitosha kuwapa wenyeji, Saint George ushindi wa 1-0 dhidi ya AS Vita.
Pamoja na matokeo hayo, vigogo hao wa Tunisia wanabaki kileleni mwa Kundi A wakiongoza kwa pointi tatu zaidi kufuatia ushindi wa Ferroviario Beira nyumbani mjini Maputo.
Baada ya kipindi cha kwanza kigumu, Zied Boughattas akawafungia bao la kwanza washindi hao wa mwaka 2007 wa Ligi ya Mabingwa bao la kuongoza dakika ya 57.
Timu ya Sudan ikafanikiwa kucheza mechi ya 24 bila kupoteza kwenye mashindano yote, baada ya kusawazisha bao hilo dakika ya 80 kupitia kwa Mohamed Musa mjinii Sousse.
MATOKOE YOTE LIGI YA MABINGWA AFRIKA
Juni 4, 2017
Al Ahly SC 2 - 0 Wydad Athletic Club
Saint George 1 - 0 AS Vita Club
Juni 3, 2017
Etoile du Sahel 1 - 1 Al-Hilal
Zanaco FC 2 - 1 Coton Sport
Ferroviario Beira 1 - 0 Al Merrikh
Juni 2, 2017
Zamalek SC 1 - 1 USM Alger
Mamelodi Sundowns 1 - 2 Esperance
CAPS United 2 - 4 Al Ahli Tripoli
0 comments:
Post a Comment