• HABARI MPYA

    Tuesday, May 16, 2017

    CHELSEA WAIPIGA WATFORD 4-3 NA KUFUMUA SHANGWE ZA UBINGWA

    Wachezaji wa Chelsea wakimrusha juu koch wao, Antonio Conte kwa furaha baada ya kujihakikishia ubingwa wa Ligi Kuu ya England kufuatia ushindi wa 4-3 dhidi ya Watford usiku wa Jumatatu Uwanja wa Stamford Bridge. Mabao ya Chelsea yalifungwa na John Terry dakika ya 22, Cesar Azpilicueta dakika ya 36, Michy Batshuayi dakika ya 49 na Cesc Fabregas dakika ya 88 wakati ya Watford yamefungwa na Etienne Capoue dakika ya 24, Daryl Janmaat dakika ya 51 na Stefano Okaka dakika ya 74. Chelsea imefikisha pointi 90 baada ya kucheza mechi 37 na sasa rasmi ni mabingwa wapya, wakirithi taji lililoachwa wazi na Leicester City PICHA ZAIDI GONGA HAPA 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: CHELSEA WAIPIGA WATFORD 4-3 NA KUFUMUA SHANGWE ZA UBINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top