• HABARI MPYA

    Thursday, February 02, 2017

    MECHI ZA WIKIENDI HII LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA

    Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo Februari 2, mwaka huu ambako Mwadui itaialika Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mwadui, Shinyanga.
    Mchezo huo pekee Na. 201 utaanza saa 10,00 jioni na Ijumaa Januari 3, Young Africans ya Dar es Salaam, itaikaribisha Stand United ya Shinyanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Jumamosi Februari 4, mwaka huu kutakuwa na mechi mbili.
    Mechi za Jumamosi  zinatarajiwa kuwa ni kati ya Mbeya City na JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya wakati Majimaji itakuwa mwenyeji wa Simba katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
    Jumapili kutakuwa na mchezo kati ya Azam FC na Ndanda FC kwenye Uwanja wa Chamazi ulioko Mbande – mchezo unaotarajiwa kuanza saa 1.00 usiku.
    Jumatatu kutakuwa na mchezo mmoja tu ambako Toto Africans ya Mwanza itaikaribisha Ruvu Shooting ya Pwani kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
    Wikiendi ya Februari 10, 11 na 12 hakutakuwa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom badala yake wawakilishi wa Tanzania katika mchuano ya kimataifa Young Africans (Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika - CL) na Azam (Kombe la Shirikisho - CC) watakuwa na mechi na mechi za kimataifa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MECHI ZA WIKIENDI HII LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top