Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
TAMASHA la Sauti za Busara 2017 liko tayari kutikisa tasnia ya muziki wa Afrika kwa mfufulizo wa vikao vyenye lengo la kukuza mafunzo ya sanaa. Wataalamu kutoka Dar es Salaam na Dakar watakutanishwa na Movers & Shakers na kutoa nafasi kwa viongozi wa tasnia ya muziki kukutana na kubadilisha mawazo ya kitaalama.
Ijumaa kutakua na mada inayohusu fursa za mitandaoni, changamoto na vitisho vinavuyoigusa tasnia ya muziki. Kutoka kwenye jopo la wageni Jude Clark, mwanzilishi wa Joose Digital na Eddie Hatitye, Mkurugenzi wa Music in Africa wataongelea ujuzi wao kwenye maeneo ya hatimiliki, utandawazi, digitali, soko la muziki duniani na maswala ya teknolojia ya mitandao. Kwa kutambua uwezo wa kidigitali ni muhimu kwenye taaluma, wahudhuriaji watashuhudia nguvu ya mitandao ya kijamii ilivyo na nguvu ya kuunganisha mashabiki na wawekezaji, na kuongeza masoko kwa kutumia mitandao ya kijamii.
Wanamuziki hujikuta mstari wa mbele kwenye harakati maarufu kwa kutumia sauti zao kwa niaba ya wasiosikika. Wakati mwingine wasanii hujikuta hatarini baada ya ujumbe wa muziki wao kuwatuhumu wasikilizaji na wenye mamlaka.
Msanii anawezaje kutumia uhuru wa kuongea na kufungiwa kitaaluma? Mada ya Jumamosi itaeleza mtazamo huru wa ubunifu Afrika, ripoti imeandikwa na waandishi 25 kutoka Nchi 14 na kuchapishwa kwa ushirikiano wa Artwatch Afrika kama sehemu ya mtandao wa Arterial, wenye lengo la kulinda uhuru wa kujieleza. Jopo litajumuisha Nelson Mandela wa kundi la Sarabi Kenya, Mamou Daffe – Mkurugenzi,Tamasha la sur le Niger, Mali na Dr. Omar Abdalla Adam –Mkurugenzi, Bodi ya Udhibiti Zanzibar.
Jumapili wasanii wa tamasha wanakaribishwa kwa maswali na majibu ya kina. Washiriki wanatarajiwa kuwa Pat Thomas and Kyekyeku kutoka Ghana, Roland Tchakounte kutoka Cameroun, Bi Mariam Hamdani kutoka Zanzibar and Sahra Halgan kutoka Somaliland. Hii ni sehemu ya kipekee kwa wasanii kutoka bara la Afrika na sehemu mbalimbali kukutana na kubadilishana mawazo. Mada hii itaongozwa na Journey Ramadhan, meneja wa Tamasha.
Movers & Shakers imeandaliwa kutengeneza nafasi za kipekee kwa wasanii na kuwajengea uwezo ili tasnia ya muziki Afrika Mashariki isonge mbele. Mada zitatolewa kila siku kuanzia saa 8:00 mchana mpaka saa 9:30 jioni . Hotel ya Monsoon. Kuingia ni kwa mwaliko tu. Hovyo wasanii na mameneja wa ndani wanahamasishwa kuwasiliana na waandaaji wa tamasha la Sauti za Sauti za Busara kama watapenda kushiriki.
Tamasha la Sauti za Busara 2017 limedhaminiwa na: Ubalozi wa Norway, Shirika la Uswis la Ushirikiana na Maendeleo (SDC), ZANTEL, Africalia, Ubalozi wa Ujerumani, Zanlink, Memories of Zanzibar, Ethiopian Airlines, Mozeti, Coastal Aviation, Ikala Zanzibar Stone Town Lodge, Music in Africa, Chuchu FM Radio, Tifu TV na Zanzibar Media Corporation.
TAMASHA la Sauti za Busara 2017 liko tayari kutikisa tasnia ya muziki wa Afrika kwa mfufulizo wa vikao vyenye lengo la kukuza mafunzo ya sanaa. Wataalamu kutoka Dar es Salaam na Dakar watakutanishwa na Movers & Shakers na kutoa nafasi kwa viongozi wa tasnia ya muziki kukutana na kubadilisha mawazo ya kitaalama.
Ijumaa kutakua na mada inayohusu fursa za mitandaoni, changamoto na vitisho vinavuyoigusa tasnia ya muziki. Kutoka kwenye jopo la wageni Jude Clark, mwanzilishi wa Joose Digital na Eddie Hatitye, Mkurugenzi wa Music in Africa wataongelea ujuzi wao kwenye maeneo ya hatimiliki, utandawazi, digitali, soko la muziki duniani na maswala ya teknolojia ya mitandao. Kwa kutambua uwezo wa kidigitali ni muhimu kwenye taaluma, wahudhuriaji watashuhudia nguvu ya mitandao ya kijamii ilivyo na nguvu ya kuunganisha mashabiki na wawekezaji, na kuongeza masoko kwa kutumia mitandao ya kijamii.
Wanamuziki hujikuta mstari wa mbele kwenye harakati maarufu kwa kutumia sauti zao kwa niaba ya wasiosikika. Wakati mwingine wasanii hujikuta hatarini baada ya ujumbe wa muziki wao kuwatuhumu wasikilizaji na wenye mamlaka.
Msanii anawezaje kutumia uhuru wa kuongea na kufungiwa kitaaluma? Mada ya Jumamosi itaeleza mtazamo huru wa ubunifu Afrika, ripoti imeandikwa na waandishi 25 kutoka Nchi 14 na kuchapishwa kwa ushirikiano wa Artwatch Afrika kama sehemu ya mtandao wa Arterial, wenye lengo la kulinda uhuru wa kujieleza. Jopo litajumuisha Nelson Mandela wa kundi la Sarabi Kenya, Mamou Daffe – Mkurugenzi,Tamasha la sur le Niger, Mali na Dr. Omar Abdalla Adam –Mkurugenzi, Bodi ya Udhibiti Zanzibar.
Jumapili wasanii wa tamasha wanakaribishwa kwa maswali na majibu ya kina. Washiriki wanatarajiwa kuwa Pat Thomas and Kyekyeku kutoka Ghana, Roland Tchakounte kutoka Cameroun, Bi Mariam Hamdani kutoka Zanzibar and Sahra Halgan kutoka Somaliland. Hii ni sehemu ya kipekee kwa wasanii kutoka bara la Afrika na sehemu mbalimbali kukutana na kubadilishana mawazo. Mada hii itaongozwa na Journey Ramadhan, meneja wa Tamasha.
Movers & Shakers imeandaliwa kutengeneza nafasi za kipekee kwa wasanii na kuwajengea uwezo ili tasnia ya muziki Afrika Mashariki isonge mbele. Mada zitatolewa kila siku kuanzia saa 8:00 mchana mpaka saa 9:30 jioni . Hotel ya Monsoon. Kuingia ni kwa mwaliko tu. Hovyo wasanii na mameneja wa ndani wanahamasishwa kuwasiliana na waandaaji wa tamasha la Sauti za Sauti za Busara kama watapenda kushiriki.
Tamasha la Sauti za Busara 2017 limedhaminiwa na: Ubalozi wa Norway, Shirika la Uswis la Ushirikiana na Maendeleo (SDC), ZANTEL, Africalia, Ubalozi wa Ujerumani, Zanlink, Memories of Zanzibar, Ethiopian Airlines, Mozeti, Coastal Aviation, Ikala Zanzibar Stone Town Lodge, Music in Africa, Chuchu FM Radio, Tifu TV na Zanzibar Media Corporation.
0 comments:
Post a Comment