• HABARI MPYA

    Thursday, January 19, 2017

    YANGA NA ASHANTI JUMAMOSI, SIMBA NA POLISI JUMAPILI KOMBE LA TFF

    Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
    YANGA SC wataanza kutetea Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC) kwa kumenyana na Ashanti United, zote za Dar es Salaam wikiendi hii.
    Mchezo huo wa hatua ya 32 Bora umepangwa kufanyika Jumamosi Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam baada ya Ashanti kuitoa timu ngumu ya Daraja la Kwanza, Friends Rangers.  
    Vigogo wengine, Simba SC watashuka Uwanja wa Uhuru Jumapili kumenyana na Polisi Dar es Salaam, wakati washindi wa pili wa mwaka jana, Azam FC watamenyana na Cosmopolitan Jumatatu Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
    Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa jioni hii na TFF, mechi nyingine za Jumamosi ni kati ya Alliance na Mbao FC Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, Maji Maji na Mighty Uwanja Maji Maji, Songea, wakati Jumapili mbali na Simba na Polisi Dar, Ruvu Shooting itamenyana na Kiluvya United Uwanja Mabatini, Toto Africans na Mwadui Uwanja wa CCM Kirumba na Mbeya Worriors na Prisons Uwanja Sokoine, Mbeya. 
    Mbali na Azam na Cosmo, mechi nyingine za Jumatatu ni kati ya Stand United na Polisi Mara Uwanja Karume, Musoma, Ndanda FC na Mlale JKT Uwanja Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, wakati Jumanne Mtibwa Sugar watamenyana na Polisi Moro Uwanja wa Uwanja Jamhuri, Morogoro, Kurugenzi FC na JKT Ruvu Uwanja wa Mafinga, Mbeya City na Kabela City Uwanja Sokoine, Madini na Panone Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
    Hatua ya 32 Bora itakamilishwa kwa mechi mbili Jumatano, Singida United wakiikaribisha Kagera Sugar Uwanja wa Namfua, Singida na African Lyon na Mshikamano Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam. Hata hivyo, mchezo wa Lyon na Mshikamano unaweza kusogezwa mbele ikibidi.

    RATIBA KAMILI 32 BORA ASFC
    Januari 21, 2017
    Alliance Vs Mbao (CCM Kirumba, Mwanza) 
    Maji Maji Vs Mighty (Maji Maji, Songea) 
    Yanga Vs Ashanti United (Uhuru, Dar es Salaam) 
    Januari 22, 2017
    Ruvu Shooting Vs Kiluvya United (Mabatini, Mlandizi) 
    Toto Africans Vs Mwadui (CCM Kirumba, Mwanza) 
    Simba SC Vs Polisi Dar (Uhuru, Dar es Salaam)
    Mbeya Worriors Vs Prisons (Sokoine, Mbeya) 
    Januari 23, 2017
    Stand United Vs Polisi Mara (Karume, Musoma) 
    Azam FC Vs Cosmopolitan (Azam Complex, Chamazi) 
    Ndanda FC Vs Mlale JKT (Nangwanda Sijaona, Mtwara) 
    Januari 24, 2016
    Mtibwa Sugar Vs Polisi Moro (Jamhuri, Morogoro) 
    Kurugenzi FC Vs JKT Ruvu (Mafinga, Iringa) 
    Mbeya City Vs Kabela City (Sokoine, Mbeya) 
    Madini Vs Panone (Sheikh Amri Abeid, Arusha) 
    Januari 25, 2017
    Singida United Vs Kagera Sugar (Namfua, Singida) 
    African Lyon Vs Mshikamano (Uhuru, Dar es Salaam)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA NA ASHANTI JUMAMOSI, SIMBA NA POLISI JUMAPILI KOMBE LA TFF Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top