• HABARI MPYA

    Sunday, December 04, 2016

    NI NIGERIA TENA MABINGWA AWCON 2017

    BAO pekee la mshambuliaji Desire Oparanozie zikiwa zimesalia dakika tano mchezo kumalizika, limeipa ushindi wa 1-0 Nigeria dhidi ya wenyeji Cameroon Jumamosi katika fainali ya Kombe la Mataufa ya Afrika kwa Wanawake (AWCON) Uwanja wa Ahmadou Ahidjo mjini Yaounde.
    Oparanozie aliyefunga pia bao la ushindi katika Nusu Fainali dhidi ya Afrika Kusini siku nne zilizotangulia mjini Limbe, aliwanyamazisha mashabiki wa nyumbani wapatao 40,000 waliofurika uwanjani.
    Inakuwa mara ya tatu kwa Nigeria kuifunga Cameroon katika fainali baada ya mwaka 2004 na 2014.
    Na ushindi huo unaifanya Nigeria iwe nchi iliyotwaa mataji mengi y AWCON bada ya awali kutwaa katika miaka ya 1998, 2000, 2002, 2002, 2006, 2010 na 2014.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI NIGERIA TENA MABINGWA AWCON 2017 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top