Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
MCHEZO wa kirafiki wa kimataifa kati ya wenyeji, Zimbabwe na Tanzania kesho utaonyeshwa moja kwa moja na Televisheni ya taifa ya nchi hiyo, ZBC.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas aliyeongozana na Taifa Stars nchini Zimbabwe, amesema kwamba timu ZBC nao wameipa haki Azam TV ya Tanzania kuonyesha pia mchezo pia.
"Kituo cha Televisheni ya Taifa hapa Zimbabwe (ZBC) na huko nyumbani wataungana na Kituo cha Televisheni cha Azam ( Azam Tv) inayopatikana kwenye king'amuzi cha Azam muda wote wa mchezo kuonyesha mchezo huo," alisema Alfred Lucas.
Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta ataiongoza timu kesho Uwanja wa Taifa wa Harare kumenyana na wenyeji, Zimbabwe katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa
Taifa Stars itashuka kwenye Uwanja wa Taifa wa Harare kesho jioni kumenyana na wenyeji, Zimbabwe katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa.
Stars imefikia kwenye hoteli ya The Rainbow Towers mjini Harare na mchezo wa kesho utaanza Saa 9.00 Alasiri kwa saa za Zimbabwe, sawa na saa 10.00 jioni kwa saa za Tanzania.
MCHEZO wa kirafiki wa kimataifa kati ya wenyeji, Zimbabwe na Tanzania kesho utaonyeshwa moja kwa moja na Televisheni ya taifa ya nchi hiyo, ZBC.
Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas aliyeongozana na Taifa Stars nchini Zimbabwe, amesema kwamba timu ZBC nao wameipa haki Azam TV ya Tanzania kuonyesha pia mchezo pia.
"Kituo cha Televisheni ya Taifa hapa Zimbabwe (ZBC) na huko nyumbani wataungana na Kituo cha Televisheni cha Azam ( Azam Tv) inayopatikana kwenye king'amuzi cha Azam muda wote wa mchezo kuonyesha mchezo huo," alisema Alfred Lucas.
Nahodha wa Taifa Stars, Mbwana Samatta ataiongoza timu kesho Uwanja wa Taifa wa Harare kumenyana na wenyeji, Zimbabwe katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa
Taifa Stars itashuka kwenye Uwanja wa Taifa wa Harare kesho jioni kumenyana na wenyeji, Zimbabwe katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa.
Stars imefikia kwenye hoteli ya The Rainbow Towers mjini Harare na mchezo wa kesho utaanza Saa 9.00 Alasiri kwa saa za Zimbabwe, sawa na saa 10.00 jioni kwa saa za Tanzania.
0 comments:
Post a Comment