TIMU ya Zesco United ya Zambia leo inaikaribisha Asec Mimosa ya Ivory Coast katika mchezo wa Kundi A Ligi ya Mabingwa Afrika.
Zesco na ASEC zote kila moja ina pointi tatu baada ya kushinda mechi moja na kufungwa moja katika Raundi mbili za awali na kila moja itahitaji kushinda leo ili kufufua matumaini ya kwenda Nusu Fainali.
Mchezo mwingine wa kundi hilo, Al Ahly ya Misri itakuwa mwenyeji wa vinara wa kundi, Wydad Casablanca ya Morocco.
Wydad inaongoza kundi hilo kwa pointi zake sita, wakati Ahly haina pointi baada ya kufungwa mechi zote za mwanzo na inashika mkia kundini.
Kundi B, Zamalek ya Misri kesho watakuwa wenyeji wa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, wakati Enyimba watakuwa mapumzikoni.
Ikumbukwe ES Setif ya Algeria iliondolewa kwenye mashindano hayo katika Kundi B baada ya vurugu za mashabiki wake.
Zesco na ASEC zote kila moja ina pointi tatu baada ya kushinda mechi moja na kufungwa moja katika Raundi mbili za awali na kila moja itahitaji kushinda leo ili kufufua matumaini ya kwenda Nusu Fainali.
Mchezo mwingine wa kundi hilo, Al Ahly ya Misri itakuwa mwenyeji wa vinara wa kundi, Wydad Casablanca ya Morocco.
Zesco United wanaikaribisha ASEC Mimosa leo Ligi ya Mabingwa |
MISIMAMO YA MAKUNDI LIGI YA MABINGWA AFRIKA
Kundi A
Na | Timu | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Wydad Casablanca | 2 | 2 | 0 | 0 | 3 | 0 | 3 | 6 |
2 | ASEC Mimosas | 2 | 1 | 0 | 1 | 2 | 2 | 0 | 3 |
3 | Zesco United | 2 | 1 | 0 | 1 | 3 | 4 | -1 | 3 |
4 | Al Ahly | 2 | 0 | 0 | 2 | 3 | 5 | -2 | 0 |
Kundi B
Na | Timu | P | W | D | L | GF | GA | GD | Pts |
1 | Mamelodi Sundowns | 1 | 1 | 0 | 0 | 2 | 1 | 1 | 3 |
2 | Zamalek | 1 | 1 | 0 | 0 | 1 | 0 | 1 | 3 |
3 | Enyimba | 2 | 0 | 0 | 2 | 1 | 3 | -2 | 0 |
Wydad inaongoza kundi hilo kwa pointi zake sita, wakati Ahly haina pointi baada ya kufungwa mechi zote za mwanzo na inashika mkia kundini.
Kundi B, Zamalek ya Misri kesho watakuwa wenyeji wa Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, wakati Enyimba watakuwa mapumzikoni.
Ikumbukwe ES Setif ya Algeria iliondolewa kwenye mashindano hayo katika Kundi B baada ya vurugu za mashabiki wake.
0 comments:
Post a Comment