• HABARI MPYA

    Friday, January 08, 2016

    SAMATTA NDIYE MWANASOKA BORA ANAYECHEZA AFRIKA, AUBAMEYANG AMBWAGA YAYA TOURE

    ORODHA KAMILI YA WASHINDI
    MCHEZAJI BORA WA AFRIKA - Pierre-Emerick AUBAMEYANG (Gabon)
    MCHEZAJI BORA ANAYECHEZA AFRIKA – Mbwana Aly SAMATTA
    MCHEZAJI BORA WA KIKE - Gaelle ENGANAMOUIT (Cameroon)
    MCHEZAJI BORA KIJANA - Victor OSIMHEN (Nigeria)
    MCHEZAJI BORA ANAYECHIPUKIA VIZURI - Etebo Peter OGHENEKARO (Nigeria)
    KOCHA BORA WA MWAKA- Herve RENARD (Ufaransa) – Kocha wa zamani wa Ivory Coast
    REFA BORA WA MWAKA - Bakary Papa GASSAMA (Gambia)
    TIMU BORA YA TAIFA – Ivory Coast
    TIMU BORA YA TAIFA YA WANAWAKE- Cameroon
    KLABU BORA YA MWAKA - TP Mazembe (DRC)
    GWIJI WA AFRIKA - Charles Kumi GYAMFI (Ghana)
    Samuel MBAPPE LEPPE (Cameroon)

    KIKOSI BORA AFRIKA
    Kipa: Robert Muteba KIDIABA (DRC)
    Mabeki: Serge AURIER (Ivory Coast), Aymen ABDENNOUR (Tunisia), Mohamed MEFTAH (Algeria)
    Viungo: Andre AYEW (Ghana), Yaya TOURE (Ivory Coast), Sadio MANE (Senegal), Yacine BRAHIMI (Algeria),     
    Washambuliaji: Mbwana Aly SAMATTA (Tanzania), Pierre-Emerrick AUBAMEYANG (Gabon), Baghdad BOUNEDJAH (Algeria) 

    WACHEZAJI WA AKIBA;
    Djigui DIARRA (Mali)
    Azubuike OKECHUKWU (Nigeria)
    Kelechi NWAKALI (Nigeria)
    Zinedine FERHAT (Algeria)
    Adama TRAORE (Mali)
    Victor OSIMHEN (Nigeria)
    Kermit ERASMUS (Afrika Kusini)
    Mbwana Samatta akipokea tuzo yake ukumbi wa mikutano wa kimataifa mjini Abuja

    Na Mwandishi Wetu, ABUJA
    MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora Anayecheza Afrika katika sherehe zilizofanyika usiku huu ukumbi wa mikutano wa Kimataifa mjini Abuja.
    Samatta amepata pointi 127, mbele ya mchezaji mwenzake wa TP Mazembe, kipa Robert Muteba Kidiaba wa DRC, aliyepata pointi 88, wakati mshambuliaji wa Etoile du Sahel ya Tunisia na timu ya taifa ya Algeria, Baghdad Bounedjah amepata pointi 63.
    Mafanikio ya Samatta anayeweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kushinda tuzo kubwa ya Afrika, yanakuja baada ya kuiwezesha Mazembe kutwaa taji la tano la Ligi ya Mabingwa Afrika, huku akiibuka mfungaji bora kwa mabao yake nane. 
    Mshambuliaji wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang ameshinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa mara ya kwanza. 
    Mchezaji wa Borussia Dortmund ya Ujerumani mwenye umri wa miaka 26, amewaangusha Yaya Toure wa Ivory Coast aliyekuwa anashikilia tuzo hiyo na Andre Ayew wa Ghana.
    Amekusanya pointi 143, saba zaidi ya Toure wakati Ayew ameshika nafasi ya tatu kwa kupata pointi 112 na anakuwa mchezaji wa kwanza wa 
    Gabon kushinda tuzo ya CAF
    Kiungo wa Nigeria, Etebo Peter Oghenekaro ameshinda tuzo ya Mchezaji Anayechipukia Vizuri dhidi ya Mnigeria mwenzake, Azubuike Okechukwu, kipa wa Mali, Djigui Diarra, Mahmoud Abdelmonem Abdelhamid ‘Kahraba’ wa Misri na Mualgeria, Zinedine Ferhat.

    Pierre-Emerick Aubameyang (kushoto) akipokea tuzo yake kutoka kwa Rais wa CAF, Issa Hayatou PICHA ZAIDI GONGA HAPA

    Etebo, anayechezea timu ya Ligi Kuu ya Nigeria, Warri Wolves, aling’ara katika michuano ya U-23 ya Afrika Desemba nchini Senegal, akiibuka mfungaji bora kwa mabao yake matano, yakiwemo mawili aliyofunga katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Algeria katika fainali.
    Mshambuliaji kinda wa Nigeria, Victor Osimhen ameshinda tuzo ya Mwanasoka Bora Chipukizi akimshinda ndugu yake, Kelechi Nwakali, wachezaji wawili wa Mali, Adama Traore na Samuel Diarra na Yaw Yeboah wa Ghana.
    Osimhen anayeshinda tuzo hiyo siku tisa tangu asherehekee kufikisha miaka 17 ya kuzaliwa, mafanikio hayo yanafuatia kufanya kwake vizuri katika Kombe la Dunia la U-17 Oktoba mwaka jana nchini Chile, akifunga mabao 10 na kuibuka mfungaji bora sambamba na kushinda Mpira wa Fedha baada ya Mchezaji Bora wa pili wa michuano hiyo, huku Nigeria ikitwaa Kombe.
    Anakuwa mchezaji wa pili wa Nigeria kushinda tuzo hiyo baada ya Kelechi Iheanacho mwaka jana.
    Mfaransa, Herve Renard ameshinda tuzo ya kocha bora wa mwaka kwa mara ya pili, baada ya kuipa Ivory Coast ubingwa wa Afrika mwaka jana nchini Equatorial Guinea.
    Mfaransa huyo amewashinda Baye Ba wa Mali U-17, Patrice Carteron wa TP Mazembe, Faouzi Benzarti wa Etoile du Sahel na Emmanuel Amunike wa Nigeria U-17.
    Samatta akiwa na Aubameyang katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa Abuja leo kabla ya kutangazwa washindi

    Renard, ambaye alishinda tuzo ya kwanza baada ya kuipa Zambia ubingwa wa Afrika mwaka 2012, alikabidhiwa tuzo yake na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya CAF, Adoum Djibrine.
    Cameroon imezishinda Ghana, Afrika Kusini na Zimbabwe katika kipengele cha timu bora ya taifa ya wanawake, wakati Ivory Coast imeziangusha 
    Ghana, Mali U-17, Nigeria U-17 na Nigeria U-23 katika timu bora ya taifa ya wanaume.
    Refa wa Gambia, Papa Bakary Gassama ameshinda tuzo ya refa bora kwa mara ya pili mfululizo akiwaangusha Ghead Zaglol Grisha wa Misri, Janny Sikazwe wa Zambia na Eric Arnaud Otogo Castane wa Gabon. 
    Mualgeria, Haimoudi Djamel pia alishinda tuzo hiyo mara mbili mfululizo mwaka 2012 na 2013.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SAMATTA NDIYE MWANASOKA BORA ANAYECHEZA AFRIKA, AUBAMEYANG AMBWAGA YAYA TOURE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top