IMEWEKWA JULAI 6, 2013 SAA 8:14 MCHANA
KLABU ya Tottenham imekamilisha usajili wa kiungo Paulinho kutoka Corinthians kwa ada ya Pauni Milioni 17.1.
Spurs imetangaza leo asubuhi kwamba, kiungo hiyo Mbrazil mwenye umri wa miaka 24 amekamilisha upimaji wa afya katika klabu hiyo.
Paulinho amesema: "Nina furaha sana ninayevutiwa na kuhamia Spurs. Ni kitu kizuri katika maisha yangu ya soka kuwa katika klabu kunwa kama Tottenham,".
Sura nzuri: Tottenham imethibitisha usajili wa Paulinho kutoka Corinthians
Paulinho akionyesha uwezo wake katika picha hii iliyopatikana kwenye tovuti ya Tottenham
Poulinho alikuwemo kwenye kikosi cha Brazil kilichotwaa Kombe la Mabara Jumapili iliyopita kwa kuifunga 3-0 Hispania katika Fainali Uwanja wa Maracana.